SiasaCanada
Canada kulitambua Taifa la Palestina mwezi Septemba
31 Julai 2025Matangazo
Canada imetoa tangazo hilo jana Jumatano, baada ya Ufaransa kusema wiki iliyopita kwamba italitambua taifa hilo na kufuatiwa na Uingereza siku moja baadaye.
Carney amesema hatua hiyo inafuatia hakikisho la mara kwa mara kutoka kwa Mamlaka ya Palestina, inayowakilisha Palestina katika Umoja wa Mataifa, kwamba wako tayari kurekebisha utawala na kufanya uchaguzi mwaka 2026 ambao hautalijumuisha kundi la Hamas.
Israel kupitia Wizara ya Mambo ya Nje imekosoa vikali tangazo hilo la Canada, huku Rais wa Mamlaka ya Palestina Mahmoud Abbas akilikaribisha kwa kuitaja kuwa ni hatua ya "kihistoria".