MigogoroAsia
Makubaliano ya kusitisha vita Thailand, Cambodia yatekelezwa
29 Julai 2025Matangazo
Msemaji wa jeshi la Thailand Winthai Suwaree alisema baada ya kuanza kwa muda wa makubaliano, nchi yake ilibaini mashambulizi ya kijeshi katika maeneo kadhaa. Hata hivyo Wizara ya ulinzi ya Cambodia imesisitiza kuwa hakujawa na mashambulizi yoyote ya kijeshi mahali popote kati ya nchi hizo mbili.
Muda mfupi baadaye jeshi la Thailand limeripoti kuwa hali ni shwari baada ya makamanda wa pande zote mbili kukutana. Cambodia na Thailand zimekuwa katika mzozo wa mpaka. Mapigano ya hivi karibuni ambayo sasa yamesimama, yalianza Alhamisi baada ya mlipuko wa bomu la kutegwa ardhini uliowauwa wanajeshi sita wa Thailand kwenye eneo la mpaka.