BUNGE KUDHIBITIWA NA WASHIA NCHINI IRAQ
14 Februari 2005Matangazo
Wakurdi nao pia wametumia ushawishi wao mzito katika uchaguzi huo wa kihistoria wa tarehe 30 mwezi wa Januari kushinikiza madai yao ya kupatiwa mojawapo ya nyadhifa kuu za taifa pamoja na mji unaogombaniwa unaozalisha mafuta wa Kirkuk.
Lakini orodha ya wagombea iliowasilishwa na Iyad Alawi Waziri Mkuu wa mpito tokea watawala wa Marekani walipokabidhi madaraka kwa wananchi wa Iraq hapo mwezi wa Juni ameweza kujipatia asilimia 13. 8 tu ya kura.