Boniface Mwangi ashtakiwa kumiliki risasi kinyume cha sheria
21 Julai 2025Matangazo
Polisi ilimkamata Mwangi, mwenye umri wa miaka 42, siku ya Jumamosi na kusema wamepata ushahidi kutoka nyumbani kwake, ikiwa ni pamoja na mabomu ya kutoa machozi ambayo bado hayajatumika, simu mbili za mkononi, kompyuta na vijitabu kadhaa vya kutunza kumbukumbu.
Mwanaharakati Boniface Mwangi akamatwa mjini Nairobi
Vijana wa kenya maarufu kama Gen Z waliokasirishwa na hali ya uchumi kudorora nchini humo wamekuwa wakiandamana mara kwa mara kupinga hali hiyo, rushwa na vitendo vya ukatili wapolisi dhidi yao.
Vijana hao wamekuwa wakitaka mageuzi serikalini ikiwa ni pamoja na kumtaka rais Ruto kun'gatuka madarakani.