UchumiAfrika
Bill Gates atangaza kuipatia Afrika Dola bilioni 200
3 Juni 2025Matangazo
Gates, ambaye Mei 8 alisema kuwa ataufunga wakfu huo ifikapo mwaka 2045, ametoa ahadi hiyo alipokuwa akiwahutubia viongozi wa Afrika mjini Addis Ababa, Ethiopia.
Amewaambia viongozi hao sehemu kubwa ya fedha hizo zitaelekezwa katika utatuzi wa changamoto barani Afrika, huku akiwahimiza kuimarisha sekta za afya na maendeleo kupitia ushirikiano na uvumbuzi.
Aidha aliyataja mataifa ya Ethiopia, Msumbiji, Nigeria, Rwanda, Zambia na Zimbabwe kama mifano ya nchi zilizoonyesha uongozi thabiti unaokuza uvumbuzi.