BERLIN Baraza la uongozi lakutana
31 Mei 2005Matangazo
Wiki moja baada ya Kansela wa Ujerumani bwana Gehard Schröder kutangaza kufanyika kwa uchaguzi mkuu mapema kabla ilivyopangwa, baraza la uongozi la vyama tawala vya SDP na Kijani limekutana leo mjini Berlin.
Wajumbe wa baraza hilo wanazungumzia juu ya sheria zinazowezwa kupitishwa bungeni katika kipindi cha wiki nne zijazo.
Pamoja na sheria hizo ni ile inayohusu kupunguza kodi za wajasiriamali
Wajumbe hao pia watazungumzia mkakati utakaotumiwa na Kansela Schröder katika kuwasilisha kura ya imani tarehe mosi julai katika bunge.
.