Bardella: Maandamano yaliopangwa sio njama dhidi ya mahakama
2 Aprili 2025Matangazo
Alipoulizwa kuhusu maandamano yaliopangwa kufanyika siku ya Jumapili kupinga uamuzi huo wa mahakama, Bardella amewaambia waandishi wa habari katika bunge la Ulaya ambapo pia anahudumu kama mbunge, kwamba maandamano hayo sio njama.
Bardella asema maandamano ni utetezi wa demokrasia ya Ufaransa
Bardella ameongeza kuwa kinyume chake, ni utetezi wa wazi na wa kina wa uongozi wa sheria na demokrasia ya Ufaransa.
Marine Le Pen apatikana na hatia katika kesi ya ubadhirifu
Bardella amesema hukumu hiyo haijabadilisha chochote katika uhusiano wake na Le Pen na akaongeza kuwa imewaleta pamoja zaidi.
Pia amesema kuwa yuko upande wa Le pen na hilo halitabadilika.