Baraza la Usalama lawajia juu waasi wa Sudan kuunda serikali
27 Februari 2025Mwakilishi wa Marekani kwenye Baraza hilo, John Kelley, alisema hatua hiyo haisaidii kurejesha amani na inatishia kuigawa Sudan.
Balozi wa Uingereza, Barbara Woodward, alielezea wasiwasi wake akitaka umoja na mamlaka ya Sudan kuheshimiwa.
Kauli kama hizo zilitolewa pia na wajumbe wa Ufaransa na China, huku naibu balozi wa Algeria, Toufik Laid Koudri, akizungumza kwa niaba ya nchi yake, Somalia, Sierra Leone na Guyana, aliwataka waasi hao kuweka mbele haja ya umoja na maslahi ya Sudan kuliko matakwa yao binafsi.
Soma zaidi: RSF na washirika wao waripotiwa kusaini hati ya kuunda serikali pinzani
Siku ya Jumapili, waasi wa RSF na washirika wao walikubaliana kuunda serikali hasimu katika mkutano uliofanyika Nairobi, hatua iliyochochea mzozo kati ya Sudan na Kenya.
Pande zilizosaini makubaliano hayo zilisema "serikali ya amani na umoja" itatawala maeneo yanayodhibitiwa na waasi nchini Sudan.