SiasaAsia
Bangladesh yasitisha usajili wa chama cha Hasina
13 Mei 2025Matangazo
Afisa wa ngazi ya juu wa tume hiyo amesema uamuzi huo umetokana na pendekezo lililotolewa na wizara ya mambo ya ndani ya nchi hiyo.
Inafuatia uamuzi wa serikali wa siku ya Jumapili wa kuzuia shughuli za chama hicho hadi mahakama itakapotoa uamuzi kuhusiana na kesi ya ukandamizaji uliofanywa na dola dhidi ya waandamanaji mwaka uliopita.
Ukandamizaji huo ambao Umoja wa Mataifa unakadiria ulisababisha vifo vya watu 1,400 kati ya mwezi Julai hadi Agosti 2024, ndio uliokuwa sababu ya kuangushwa utawala wa Hassina.
Chama cha Awami League ndio kikongwe zaidi nchini Bangladesh na kiliitawala nchi hiyo tangu ilipopata uhuru mwaka 1971.