SiasaAfrika Kusini
Balozi wa Afrika Kusini asema hajutii kurudi kwake nyumbani
23 Machi 2025Matangazo
Ebrahim Rasool amewaambia mamia ya Waafrika Kusini mjini Cape Town kuwa halikuwa chaguo lake kurudi nyumbani, lakini hajutii kurudi kwake nyumbani. Rasool alitimuliwa kutoka Washington kwa tuhuma za kuwa "mwanasiasa mbabe" anayemchukia Trump na nchi ya Marekani.
Balozi Ebrahim Rasool, mwanaharakati wa zamani wa kupinga ubaguzi wa rangi, amesema uhusiano uliokuwepo zamani wa kufanya biashara na Marekani hautafanya kazi.
Uhusiano kati ya Washington na Pretoria umedorora tangu Trump kukata msaada wa kifedha kwa Afrika Kusini kutokana na kile anachodai ni sera ya Pretoria inayoruhusu ardhi kutekwa kutoka kwa wakulima weupe.