SiasaMarekani
Baerbock ataka mabadiliko kwenye Umoja wa Mataifa
3 Juni 2025Matangazo
Baerbock aliyechaguliwa jana Jumatatu kushika wadhifa huo, alipozungumza na DW amesema Umoja wa Mataifa bado una jukumu kubwa katika kukabiliana na changamoto za amani, usalama na haki za binaadamu na kuongeza kuwa mageuzi hayo yatazirahisishia taasisi za Umoja wa Mataifa kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.
Baerbock, waziri wa zamani wa Mambo ya Nje ya Ujerumani, ni mwanamke wa tano kushika wadhifa huo.
Amezungumzia pia msukumo wa kupata Katibu Mkuu mwanamke, akiangazia dhamira pana ya usawa wa kijinsia katika majukumu ya uongozi wa Umoja wa Mataifa na kujenga maelewano baina ya nchi wanachama.