Askari polisi akamatwa Kenya kwa kumpiga risasi raia
18 Juni 2025Matangazo
Msemaji wa Polisi, Muchiri Nyaga amesema Mkuu wa Jeshi la Polisi aliamuru kukamatwa mara moja na kufikishwa mahakamani kwa askari huyo aliyefyatua risasi.
Maandamano ya kupinga mauaji ya Ojwang aliyekufa akiwa mikononi mwa polisi, yalifanyika jana Nairobi, Mombasa, Kilifi na Kwale. Tume ya Kitaifa ya Haki za Binaadamu ya Kenya, imesema watu 21 walijeruhiwa wakati wa maandamano hayo.
Mapema Jumanne, vidio iliyochapishwa katika mtandao wa kijamii wa X wa kituo cha Televisheni cha Citizen, iliwaonyesha polisi wawili wakimpiga mara kadhaa mwanaume kichwani kabla ya polisi mmoja kumpiga risasi wakati akijaribu kuondoka.
Mwanaume huyo alidondoka chini huku kundi la waandamanaji likipiga kelele wakisema "umemuua".