Araghchi: Mazungumzo na Marekani yanaendelea kusonga mbele
19 Aprili 2025Matangazo
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghchi amesema leo kwamba mazungumzo ya nyuklia kati ya Iran na Marekani yanaendelea "kusonga mbele" baada ya kufanyika mkutano alioutaja kuwa mzuri.
Mwanadiplomasia huyo wa Iran ameiambia televisheni ya serikali ya Iran kwamba mkutano uliofanyika leo ulikuwa mzuri na kwamba walifanikiwa kufikia uelewa bora juu ya mfululizo wa kanuni na malengo.
Soma zaidi:Mkuu wa IAEA Rafael Grossi afanya ziara mjini Tehran
Amesema duru inayofuata ya mazungumzo hayo yatafanyika mjini Muscat, Oman mnamo Aprili 26 japo wataalamu watakutana huko siku chache kabla ya kuanza kwa mazungumzo hayo.