Araghchi awasili Istanbul kushiriki mkutano wa OIC
23 Juni 2025Matangazo
Kulingana na shirika la habari la Uturuki Anadolu, mamia ya washiriki wanatarajiwa kuhudhuria mkutano huo wa siku mbili. Miongoni mwao ni mawaziri wapatao 43 na wawakilishi wa ngazi za juu wa Umoja wa Mataifa na nchi za kiarabu.
Iran yarusha makombora Israel, juhudi za kidiplomasia zaendelea Geneva
Mkutano huo unakuja siku moja baada ya Araghchi kufanya mazungumzo mjini Geneva juu ya suluhisho la kidiplomasia katikamzozo huo na mawaziri wenzake wa mambo ya nje kutoka mataifa ya Ulaya, ikiwa ni pamoja na Johann Wadephul wa Ujerumani, Jean-Noël Barrot wa Ufaransa na David Lammy wa Uingereza.