Baerbock achaguliwa Rais Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa
8 Septemba 2025Matangazo
Baerbock alipata kura 167, karibu mara mbili ya kura 88 zinazohitajika kushinda, huku mwanadiplomasia wa ngazi ya juu wa Ujerumani, Helga Schmid, akipata kura saba na mataifa mengine 14 kujizuwia kupiga kura.
Ujerumani ilikuwa imemteua Schmid kuwania nafasi ya hiyo, lakini baadaye ikampeleka Baerbock baada ya kupoteza kazi yake kama waziri wa mambo ya nje katika uchaguzi uliofanyika hivi karibuni, uamuzi uliokosolewa na baadhi ya watu ndani ya Ujerumani kwenyewe.
Hata hivyo, Urusi imemkosoa Baerbock ikisema ana sera za kuibagua Urusi, mbinafsi na asiye uelewa mzuri wa masuala ya kidiplomasia.