Ancelotti kuondoka Madrid kuwa kocha mpya wa Brazil
29 Aprili 2025Kocha wa Real Madrid Carlo Ancelotti anatarajiwa kuondoka klabu hiyo kwenda kuisimamia timu ya taifa ya soka ya Brazil hadi kombe la dunia la mwaka 2026.
Wavuti wa The Athletic umeripoti kwamba Mtaliani huyo ameshawafahamisha wachezaji kuhusu mpango wake wa kuondoka.
Anceloti anatarajiwa kusimamia kikosi cha Seleção wakati wa mechi za kimataifa mwezi Juni. Kwa maana hiyo hataweza kuiongoza Real Madrid katika mashindano ya kombe la dunia la vilabu lililopangwa kufanyika kuanzia Juni 14 hadi Julai 13 nchini Marekani.
Gazeti la michezo la Uhispania Marca limeripoti kwamba makubaliano yameshafikiwa lakini yanasubiri kutiwa saini.
Ancelotti ana mkataba na klabu ya Real Madrid hadi 2026, lakini anatarajiwa kuondoka kutokana na matokeo mabaya ya hivi karibuni ambapo Real ilitolewa nje ya kombe la mabingwa Ulaya na ikapoteza fainali ya Copa del Rey dhidi ya Barcelona.