Amorim: Niko tayari kuondoka United
22 Mei 2025Matangazo
Hii ni baada ya timu yake kushindwa katika fainali ya Ligi ya Europa dhidi ya Tottenham Hotspurs Jumatano usiku.
Brennan Johnson alifunga bao pekee muda mfupi kabla ya kipindi cha mapumziko cha mechi hiyo ya fainali iliyopigwa mjini Bilbao jana Jumatano, huku United wakishindwa kurejesha bao hilo.
Kushindwa huko kunaifanya timu hiyo kuwa na msimu mbaya hata zaidi na kumaliza katika nafasi ya 16 ambayo ni ya chini kabisa ya ligi tangu iliposhushwa daraja mwaka 1974.
Amorim aliyerithi mikoba ya Erik Ten Hag mwezi Novemba, ameshinda michezo sita tu ya ligi ya Premier, lakini bado anaamini anaweza kubadilisha hali ya mambo kwenye uga wa Old Trafford.