Amnesty yataka udhibiti vifaa vinavyotumia shoti ya umeme
6 Machi 2025Matangazo
Shirika hilo limesema vifaa hivyo vimekuwa vinatumiwa na vyombo vya dola kuwatesa na kuwadhuru watu kwenye mataifa mengi ikiwemo China, Venezuela na Iran.
Amnesty International imesema vifaa vya shoti ya umeme vimegeuka silaha kwenye jela, vituo vya watu wenye matatizo ya akili na hata kambi za wahamiaji na wakimbizi.
Limefafanua kwamba licha ya athari zilizo wazi kwa haki za binadamu bado hakuna kanuni za kimataifa zinazosimamia utengenezaji na mauzo ya vifaa vya aina hiyo duniani.
Amnesty International imetahadharisha kwamba iwapo matumizi yake hayatadhibitiwa watu wataendelea kuteseka na kunyanyaswa na maafisa wa usalama wanaovitumia kwa njia holela.