Amnesty: Wafanyikazi wakabiliwa na ubakaji Saudi Arabia
13 Mei 2025Katika ripoti yao iliyotolewa leo Jumanne, Amnesty International imeongeza kuwa masharti ya kazi kwa Wakenya hao ni ya kikatili kiasi cha kufikia kiwango cha kile walichokiita "kazi ya kulazimishwa na usafirishaji haramu.”
Shirika hilo la kutetea haki za binadamu limeeleza kwa kina hali ya mateso wanayopitia zaidi ya wanawake 70 waliokuwa wakifanya kazi za nyumbani nchini Saudi Arabia.
Soma pia: Amnesty: Haki za binadamu duniani ziko hatarini
Wafanyikazi wao wa ndani wanatajwa kupitia hali mbaya za maisha na unyanyasaji wa kibinadamu ikiwa ni Pamoja na ukatili wa kingono, matusi na vipigo.
Amnesty International pia imesema serikali ya Kenya inahusika moja kwa moja katika unyonyaji huo wa wafanyikazi.
Ripoti hiyo imetolewa wakati Rais wa Marekani Donald Trump akitarajiwa kufanya ziara rasmi leo mjini Riyadh.