MigogoroSudan
Amnesty: Silaha za China zilizosambazwa na UAE zakutwa Sudan
8 Mei 2025Matangazo
Amnesty imesema silaha hizo zilitumiwa huko Khartoum na Darfur, hatua ambayo inakiuka vikwazo vya silaha vya Umoja wa Mataifa. Hayo yakiarifiwa, Ubalozi wa China nchini Sudan umewataka raia wake kuondoka haraka iwezekanavyo nchini humo kutokana na kuzorota kwa hali ya usalama.
Tangu Aprili mwaka 2023, kundi la RSF limekuwa katika vita na jeshi la Sudan, mzozo ambao umesababisha maafa makubwa ikiwa ni pamoja na vifo vya maelfu ya watu, huku wengine wapatao milioni 13 wakilazimika kuyahama makazi yao.