AI yasema M23 wanahusika na uhalifu wa kivita
27 Mei 2025Shirika hilo la haki za binaadamu limeituhumu M23 kwa mauaji, utesaji na kuwapelekea raia kadhaa kutoweka kwenye miji miwili inayoshikiliwa na waasi hao.
Taarifa iliyotolewa na shirika hilo siku ya Jumanne (Mei 27) ilisema kuwa baina ya mwezi Februari na Aprili mwaka huu, waasi wa M23 waliwakamata, kuwauwa na kuwatesa mamia ya raia kwenye miji ya Goma na Bukavu, wakiwatuhumu kuwaunga mkono wanajeshi wa serikali.
Soma zaidi: Rais wa zamani wa DR Kongo Joseph Kabila awasili Goma
Manusura waliohojiwa na shirika hilo walielezea kiwango cha mateso walichokumbana nacho mikononi mwa M23, ingawa walisema hakukuwa na ushahidi wowote wa wao kuungana na jeshi la serikali.
Amnesty International imesema ripoti walizokusanya kutoka kwa manusura hao zinaashiria kuwa waasi hao wanaoungwa mkono na Rwanda walitenda makosa yanayolingana na uhalifu wa kivita.